Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Kigoma

KIKAO CHA KIEF TAREHE 3 DESEMBA 2017 NUR ISLAMIC MAGOMENI

Picha
Wajumbe wa KIEF wakiwa kwenye kikao cha kawaida kwa ajili ya kupanga shughuli mbali mbali za KIEF. Kikao kilifanyika tarehe 3/12/2017 kwa ajili ya maandalizi ya uzinduzi wa Mradi wa Masomo ya Ziada kwa shule za sekondari ambao umeanza tangu 16/10/2017 katika eneo la Mradi shule ya Msingi Ujiji

TAARIFA YA KUANZA KWA MRADI WA MASOMO WA KIEF TAREHE 16-10-2017

Picha
Wanafunzi wote waliochukua fomu na kuzirejesha za kujiunga na masomo ya ziada ktk Mradi unaodhaminiwa na Asasi ya KIEF mnaarifiwa kuwa masomo yataanza rasmi J umatatu Tarehe 16/10/2017 Saa 10 Jioni Shule ya Msingi Ujiji. Wanafunzi na wazazi/walezi wa wanafunzi hao mmetumiwa ujumbe kwenye Namba za simu mlizojaza kwenye fomu. Ujumbe huo umewajulisha juu ya kuchaguliwa kwenu kujiunga na program hii maalumu. KIEF inawapongeza wote walichaguliwa na pindi nafasi zikiongezeka, wale walioomba awamu hii watahudumiwa kwanza.

MHANDISI MBAROUK MAKUKA KATIKA HARAKATI ZA KULIPIA ANKARA YA TANESCO KWA AJILI YA UJIJI PRIMARY LEO TRH 12-10-2017

Picha
Picha mbalimbali zikimuonyesha Mhandisi Mbarouk Makuka wakati wa harakati ya kulipia gharama za kuunganisha umeme kwenye shule ya Msingi Ujiji iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji. Msaada wa kiasi cha Shilingi za Kitanzania 320,000 zimetolewa na wadau wa KIEF kupitia mwana KIEF Husna Sungura kwa ajili ya kugharamia mchakato huo. KIEF inatanguliza shukurani kwa Wadau wanaotuunga mkono.

MAKABIDHIANO YA MALIPO YA KUUNGANISHA UMEME SHULE YA MSINGI UJIJI LEO TRH 12-10-2017

Picha
Mapema leo hii  tarehe 12-10-2017 Mhandisi Mbarouk Makuka ,(pichani kulia) Mratibu wa muda wa Asasi ya kielimu ya Kigoma Elimu Foundation (KIEF) yenye maskani yake katika viunga vya Manispaa ya Ujiji -Kigoma akimkabidhi  Mkuu wa Shule Ndugu Moses Wilbroad (pichani kushoto) h 320,000/= kwa ajili kuvuta umeme katika majengo ya shule ya msingi Ujiji ati ya malipo ya shilingi za Tanzania Fedha hizo zimetolewa na wana Asasi hiyo ikiwa ni sehemu ya kusaidia kusukuma gurudumu la MAENDELEO ya Taaluma ya mkoa wa Kigoma. Tunakushukuruni kwa kuendelea kujinyima na kusaidia wadogo zetu waweze kufanya vema katika masomo yao.

TANGAZO LILILOBANDIKWA KWENYE MAENEO YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI

Picha
Tangazo likiwa limebandikwa kwenye 'mrangi' kwa ajili ya kuwatangazia wakazi wa Kigoma Ujiji fursa ya Masomo ya ziada wa wanafunzi wa sekondari inayoendeshwa na KIEF leo tarehe 2-10-2017

HARAKATI ZA KUBANDIKA MATANGAZO MITAA YA UJIJI LEO TRH 2-10-2017

Picha
Mjumbe wa KIEF, Mwalimu Mbaruku Makuka akibandika matangazo yanayohusu mpango wa KIEF wa masomo ya ziada kwa wanafunzi wa sekondari unaotarajiwa kuanza hivi karibuni kwenye mitaa mbali mbali ya Ujiji. Uchukuaji wa fomu za maombi umeanza leo kwenye ofisi ya KIEF iliyopo Kona ya Lumumba na Mtaa wa Buhoro Ujiji, Mkabala na uwanja wa Kawawa.

TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMO YA ZIADA KWA UDHAMINI WA KIEF

Picha
TANGAZO LA MASOMO YA ZIADA  CHINI YA UDHAMINI WA KIGOMA ELIMU FOUNDATION (KIEF)

WAKILI MSOMI WA KIEF AKIWASILISHA RASIMU YA KATIBA YA KIEF KWENYE KIKAO CHA TAREHE 27/08/2017

Picha
Wakili Msomi Ibrahim Shineni, akiwasilisha mbele ya wajumbe wa KIEF rasimu ya katiba katika kikao kilichofanyika tarehe 27/08/2017 Jijini Dar es Salaam.

WALIO MBALI HUSHIRIKI VIKAO KWA NJIA YA MTANDAO

Picha
Wajumbe wakimsikiliza kwa makini Mjumbe wa KIEF Bakari Issa alliye masomoni India akiwasilisha maoni yake kuhusu katiba ya KIEF kupitia njia ya mtandao katika kikao cha tarehe 27/08/2017. Njia hii imekuwa ikiwapa fursa walio mbali kushiriki vikao moja kwa moja kwa njia ya mtandao.

WAJUMBE WA KIEF WAKIPATA CHAKULA CHA MCHANA TAREHE 27/08/2017

Picha
Picha mbali mbali wakati wajumbe wa KIEF wakipata chakula cha mchana kabla ya kikao cha Mjadala wa Katiba kilichofanyika Nur Islamic Secondary School Magomeni tarehe 27/08/2017.

WAJUMBE WAKIFURAHIA "SELFIE" BAADA YA USAILI WA KARANI WA KIEF TAREHE 23-08-2017

Picha
Wajumbe wa KIEF, Astahili Akilimali, Husna Sungura na Ahmadi Sovu wakijiburudisha na "Selfie" baada ya kazi ya Usaili wa Karani wa KIEF uliofanyika Nur Islamic Magomeni Dar es Salaam.

USAILI WA KARANI WA KIEF ULIOENDESHWA NA JOPO LA USAILI LA KIEF TAREHE 23-08-2017

Picha
Wajumbe wa KIEF, wakiendelea na Usaili wa Karani wa KIEF atakaehudumia ofisi ya KIEF iliyopo Ujiji Kigoma, mtaa wa Lumumba/Buhoro. Mradi wa Masomo ya ziada wa KIEF ukiwa hatua za mwisho kabla ya kuanza.

FURSA YA UDHAMINI WA ASTASHAHADA YA UUGUZI NA UKUNGA KWA WASICHANA MKOA WA KIGOMA KUTOKA BMB-RTz

Picha
Tangazo la Fursa Udhamini wa Elimu kwa Wasichana wa Mkoa wa Kigoma , Elimu ya Ukunga na Uuguzi ngazi ya Astashahada. Ufadhili unaratibiwa na More and Better Midwives For Rural Tanzania. Angalia kipeperushi kwa maelezo zaidi. Mwisho wa Maombi ni Tarehe 30-08-2017

SEHEMU YA VITABU VYA KIADA VILIVYOKUSANYWA WAKATI WA KIKAO

Picha
Hivi ni sehemu ya Vitabu vya kiada vilivyokusanywa kwenye kikao cha Tarehe 13-08-2017 kilichofanyika Nur Islamic Magomeni

UPOKEAJI WA MICHANGO MBALI MBALI ILIYOTOLEWA NA WAJUMBE WA KIEF SIKU YA KIKAO TAREHE 13-08-2017

Picha
Upokeaji wa Michango mbali mbali iliyotolewa na wajumbe wa KIEF siku ya kikao tarehe 13-08-2017 pale Nur Islamic. Mradi huu hutegemea michango ya wanachama wa KIEF kwa ajili ya utekelezaji. Hapa wakikabidhi michango ya Pesa kwa ajili ya ununuzi wa thamani za Ofisi ya KIEF iliyopo Ujiji Kigoma, mtaa wa Lumumba/Buhoro.

WAJUMBE WA KIEF NA MWANDISHI NGULI SHEIKH MOHAMMED SAIDI KATIKA PICHA YA PAMOJA KABLA YA KIKAO CHA TAREHE 13-08-2017

Picha
Wajumbe wa KIEF wakiwa katika picha ya pamoja na mwandishi nguli wa vitabu na makala Sheikh Muhammed Saidi kabla ya Kikao cha KIEF kilichofanyika tarehe 13-08-2017 katika shule ya Nur Islamic iliyopo Magomeni.

MAPOKEZI YA VITABU VILIVYOTOLEWA KWA AJILI YA MRADI WA MASOMO YA ZIADA KATIKA KIKAO TAREHE 13-08-2017

Picha
Wajumbe wakipokea na kukagua vitabu vilivyotolewa na wadau kwa ajili ya mradi wa masomo ya ziada kwa wanafunzi wa Shule za Upili za Manispaa ya Kigoma Ujiji, Unaotarajiwa kuanza hivi karibu. Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa kikao cha Wiki cha KIEF kilichofanyika katika shule ya Nur Islamic magomeni.

UDAHILI WA WALIMU WATAKAOSHIRIKI KWA KUJITOLEA KWENYE MRADI WA KIEF 12-08-2017

Picha
Wajumbe wa Kigoma Elimu Foundation, wakiendelea na udahili wa Walimu watakaoshiriki mradi wa KIEF wa masomo ya ziada, unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni katika Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa wanafunzi wa Manispaa hiyo.

WAJUMBE WAKIKAGUA MEZA ILOYOTOLEWA NA MMOJA WA WANA KIEF KWA AJILI YA MRADI 30/07/2017

Picha
Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi "Mwalimu wa Kiswahili"Ahmadi Sovu akipokea meza itakayotumika kwenye mradi ofisi ya KIEF Ujiji kutoka kwa mjumbe wa KIEF Mwalimu Astahili Akilimali siku ya tarehe 30-07-2017 baada ya kikao cha Kamati ya Maandalizi

WAJUMBE WA KAMATI WAKIZIKAGUA FULANA HUSIKA 30-07/2017

Picha
Wajumbe wakizikagua fulana zitakazotumiwa na wanafunzi watakaoshiriki Mradi wa Masomo ya Ziada utakaoendeshwa na KIEF kwa wanafunzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji